- 7,336 viewsDuration: 3:00Zaidi ya watu ishirini wamekamatwa kwenye operesheni ya kiusalama iliyolenga magenge yanayowahangaisha wakazi wa maeneo kadhaa ya kaunti ya Nakuru. Operesheni hii ikiendeshwa katika mitaa ya London, Gioto na Hilton ambapo wahalifu wamekuwa wakiwavamia na kuwajeruhi wakazi. Kwa mujibu wa maafisa wa usalama, operesheni hii imefuatia visa vya wizi na uvamizi wa wakazi na madereva katika barabara ya Nakuru - Kabarak.