- 139 viewsDuration: 1:13Waziri wa utumishi wa umma na Mipango maalum, Geoffrey Ruku amezuru Kaunti ya Turkana kutathmini hali ya ukame katika eneo hilo. Hii ni kufuatia kaunti hii ya Turkana kuwa miongoni mwa Kaunti 23 zilizoathirika zaidi na kiangazi huku waakazi wakikumbwa na makali ya njaa, wafugaji wakihangaika kwa kutembea mbali kutafuta maji. Waziri Ruku anasema zaidi ya watu milioni 3.3 nchini wanakabiliwa na makali ya njaa akisema serikali kupitia halamashauri ya kukabiliana na majanga ya NDMA imeanza kutoa pesa kwa wakongwe kupitia mpango wa Inua Jamii.