Waziri Mkuu wa Haiti kujiuzulu litapoundwa baraza la mpito
Waziri Mkuu wa Haiti Ariel Henry, amesema atajiuzulu baada ya kuundwa kwa baraza la mpito la uongozi ingawa wakuu wa magenge ya uhalifu wanasisitza juu ya kuhusishwa kwenye mipango yoyote ya kuunda serikali ya mpito.
Henry alikubali kujiuzulu Jumatatu wakati wa mkutano wa dharura wa Jumuia ya Mataifa ya Caribbean nchini Jamaica, ambako Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani aliahidi msaada wa ziada wa zaidi ya dola milioni 100 kuwezesha kupelekwa kikosi cha kimataifa nchini humo.
Akizungumza kutokea Pueto Rico, Waziri Mkuu Ariel Henry amesema kufuatia mkutano wa mawaziri wa Jumuia ya Mataifa ya Caribbean CARICOM, ameamua kujiuzulu akisema Haiti inahitaji amani, utulivu na maendeleo.
Henry “Serikali ninayoiongoza itaondoka mara tu baada ya kuundwa kwa baraza la utawala. Itaendelea kufanya kazi za siku hadi siku hadi pale waziri mkuu na serikali mpya itakapoteuliwa.”
Uamuzi wa kujiuzulu kwa Henry ulitangazwa na Rais Mohamed Irfaan Ali wa Guyana, Rais wa sasa wa CARICOM, baada ya mazungumzo ya faragha ya saa kadhaa ya mawaziri wa mambo ya nje wa jumuiya hiyo yaliyohudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken.
Akizungumza kwenye mkutano huo wa Jamaica Blinken amesema kutokana na ghasia za magenge ya uhalifu kupata nguvu inadhihirisha umuhimu mkubwa wa kupelekwa kwa kikosi cha kimataifa.
Blinken amesema “kutokana na hali ya dharura inayojitokeza ninatangaza hii leo kwamba Wizara ya Ulinzi ya Marekani inaongeza maradufu msaada wake kwa kikosi hicho kutoka dola milioni 100 kufikia dola milioni 200, na hivyo kwa ujumla inafikisha msaada wa Marekani kuwa milioni 300 kwa ajili ya juhudi hiyo.
Zaidi ya hapo ninatangaza msaada wa dharura wa dola milioni 33 kusaidia huduma za afya na chakula za Haiti.”
Hata hivyo haifahamiki bado jinsi utawala wa mpito utakavyo undwa na wachambuzi wanasema haikowazi iwapo mipango hiyo ya kimataifa itaweza kutekelezwa kwani wakuu ya magenge ya uhalifu wanataka kuhusishwa kwenye utaratibu kamili.
Kiongozi wa magenge hayo Jimmy Cherizer anayejulikana kama “Barbacue” akizungumza na waandishi habari mjini Port au Prince amesema wanaitaka Jumuiya ya Kimataifa kuwapatia Wahaiti nafasi ya kujiamulia mustakbali wao.
Cherizer ‘Barbacue’ anaeleza “tunacho omba ni kuchaguliwa mtu atakaye ongoza nchi anayeishi pamoja na sisi na uamuzi kufanywa na wananchi wa Haiti. Tunataka mawaziri wote watoke katika jamii ya wahaiti.”
Haiti hivi sasa iko katika hali ya dharura tangu Machi 3 na Barbecue amewaonya wamiliki wa hoteli kuu zote kuhakikisha hawapapi hifadhi mawaziri wa serikali na kwamba watavamia hoteli moja hadi nyingine kuhakikisha jambo hilo halifanyiki. - Reuters, AFP
#rais #kenya #williamruto #wazirimkuu #Arielhenry #marekani #raiawamarekani #misaadayakibinadamu #umojawamataifa #haiti #magenge #polisi #wananchi #mauaji #wakimbizi #voa #voaswahili #carribean
12 Aug 2025
- Govt has announced privatisation plans for some of the biggest State companies.
12 Aug 2025
- Kenyans to expect temperatures as low as 8°C in some regions.
12 Aug 2025
- The former DP has been making controversial remarks.
12 Aug 2025
- Douglas Kamau says he narrowly escaped death when a bullet struck his arm and ribs, allegedly fired by a police officer from Makutano Police Station.
12 Aug 2025
- Naivasha Senior Resident Magistrate Wilson Rading on Monday recused himself from hearing the case against 73-year-old farmer Francis Muya, who is accused of plotting to kill five members of his family.
12 Aug 2025
- While Chirchir is of the opinion that road crashes are “preventable if all road users play their part” the Motorists Association of Kenya (MAK) has placed blame on government agencies.
12 Aug 2025
- The Ethics and Anti-Corruption Commission (EACC) has 9 governors on its radar over corruption cases as it intensifies its crackdown on nationwide graft.
12 Aug 2025
- Prosecutors in the Ivory Coast said Monday they have charged 11 people, including members of the opposition party of ex-president Laurent Gbagbo, with alleged "terrorist" offences linked to unrest earlier this month.
12 Aug 2025
- Authorities in Taiwan were scrambling on Tuesday to evacuate hundreds ahead of a possible landfall by Typhoon Podul on the island's southeastern coast, while nearby areas battle to recover from floods and record winds brought by previous storms.
12 Aug 2025
- Hundreds of cabin crew members took their fight to major Canadian airports on Monday, picketing against unpaid labor, as talks on wages intensify between Air Canada AC.TO and its flight attendants this week ahead of a possible strike.
12 Aug 2025
- Condemnations poured in from the United Nations, the EU and media rights groups Monday after an Israeli strike killed an Al Jazeera news team in Gaza, as Palestinians mourned the journalists and Israel accused one of them of being a Hamas militant.
12 Aug 2025
- Scientists have discovered the fossil of a tiny mouse-sized mammal that lived in the time of the dinosaurs in Chilean Patagonia.
12 Aug 2025
- Govt has announced privatisation plans for some of the biggest State companies.