Waziri Mkuu wa Haiti kujiuzulu litapoundwa baraza la mpito
Waziri Mkuu wa Haiti Ariel Henry, amesema atajiuzulu baada ya kuundwa kwa baraza la mpito la uongozi ingawa wakuu wa magenge ya uhalifu wanasisitza juu ya kuhusishwa kwenye mipango yoyote ya kuunda serikali ya mpito.
Henry alikubali kujiuzulu Jumatatu wakati wa mkutano wa dharura wa Jumuia ya Mataifa ya Caribbean nchini Jamaica, ambako Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani aliahidi msaada wa ziada wa zaidi ya dola milioni 100 kuwezesha kupelekwa kikosi cha kimataifa nchini humo.
Akizungumza kutokea Pueto Rico, Waziri Mkuu Ariel Henry amesema kufuatia mkutano wa mawaziri wa Jumuia ya Mataifa ya Caribbean CARICOM, ameamua kujiuzulu akisema Haiti inahitaji amani, utulivu na maendeleo.
Henry “Serikali ninayoiongoza itaondoka mara tu baada ya kuundwa kwa baraza la utawala. Itaendelea kufanya kazi za siku hadi siku hadi pale waziri mkuu na serikali mpya itakapoteuliwa.”
Uamuzi wa kujiuzulu kwa Henry ulitangazwa na Rais Mohamed Irfaan Ali wa Guyana, Rais wa sasa wa CARICOM, baada ya mazungumzo ya faragha ya saa kadhaa ya mawaziri wa mambo ya nje wa jumuiya hiyo yaliyohudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken.
Akizungumza kwenye mkutano huo wa Jamaica Blinken amesema kutokana na ghasia za magenge ya uhalifu kupata nguvu inadhihirisha umuhimu mkubwa wa kupelekwa kwa kikosi cha kimataifa.
Blinken amesema “kutokana na hali ya dharura inayojitokeza ninatangaza hii leo kwamba Wizara ya Ulinzi ya Marekani inaongeza maradufu msaada wake kwa kikosi hicho kutoka dola milioni 100 kufikia dola milioni 200, na hivyo kwa ujumla inafikisha msaada wa Marekani kuwa milioni 300 kwa ajili ya juhudi hiyo.
Zaidi ya hapo ninatangaza msaada wa dharura wa dola milioni 33 kusaidia huduma za afya na chakula za Haiti.”
Hata hivyo haifahamiki bado jinsi utawala wa mpito utakavyo undwa na wachambuzi wanasema haikowazi iwapo mipango hiyo ya kimataifa itaweza kutekelezwa kwani wakuu ya magenge ya uhalifu wanataka kuhusishwa kwenye utaratibu kamili.
Kiongozi wa magenge hayo Jimmy Cherizer anayejulikana kama “Barbacue” akizungumza na waandishi habari mjini Port au Prince amesema wanaitaka Jumuiya ya Kimataifa kuwapatia Wahaiti nafasi ya kujiamulia mustakbali wao.
Cherizer ‘Barbacue’ anaeleza “tunacho omba ni kuchaguliwa mtu atakaye ongoza nchi anayeishi pamoja na sisi na uamuzi kufanywa na wananchi wa Haiti. Tunataka mawaziri wote watoke katika jamii ya wahaiti.”
Haiti hivi sasa iko katika hali ya dharura tangu Machi 3 na Barbecue amewaonya wamiliki wa hoteli kuu zote kuhakikisha hawapapi hifadhi mawaziri wa serikali na kwamba watavamia hoteli moja hadi nyingine kuhakikisha jambo hilo halifanyiki. - Reuters, AFP
#rais #kenya #williamruto #wazirimkuu #Arielhenry #marekani #raiawamarekani #misaadayakibinadamu #umojawamataifa #haiti #magenge #polisi #wananchi #mauaji #wakimbizi #voa #voaswahili #carribean
15 May 2024
- CS Kindiki had earlier promised to reduce the passport waiting time to 7 days.
15 May 2024
- The incidents have raised alarm over the working relationships of the security units.
15 May 2024
- Nairobi Senator Edwin Sifuna was struggling to contain the crowd.
16 May 2024
- Reading Time: 2 minutes Under the guidance of H.E. President Wi*liam Ruto, the Ministry of Youth Affairs, Creative Economy, and Sports has received explicit […]
16 May 2024
- Reading Time: 2 minutes Persons living with disabilities are among the 3,000 households set to benefit from a three-year project meant for residents facing […]
16 May 2024
- Reading Time: < 1 minute Police in Nyahururu yesterday said employees of a second-hand clothes d****r wi*l be charged in connection with the death of […]
16 May 2024
- Reading Time: 3 minutes A group of elite athletes have been dragged into a tussle over the ownership of a matr*monial property valued at […]
16 May 2024
- Singapore on Wednesday swore in Lawrence Wong as its new prime minister Wednesday, replacing Lee Hsien Loong following two decades in office, with the new leader warning that the trade-dependent city-state faced a riskier, more conflict-ridden world.
16 May 2024
- Reading Time: < 1 minute National Council Churches of Kenya (NCCK), has urged the government to intensify the w*r on corruption, to curb theft and […]
16 May 2024
- Reading Time: 3 minutes The country has witnessed an increase in intimate partner k******s, with at least four cases reported in the past one […]
16 May 2024
- Reading Time: < 1 minute The board of the Youth Enterprise Development Fund (YEDF) has refuted reports that the Kenya Kwanza Government has deni*d it […]
16 May 2024
- United States Ambassador to Kenya Meg Whitman has dismissed claims that she is among President William Ruto’s chief advisors.
16 May 2024
- Slovak Prime Minister Robert Fico suffered life-threatening injuries on Wednesday when he was shot and wounded in an attempted assassination that stunned his small Central European nation and drew a chorus of international condemnation.