Taharuki imetanda eneo la Kibiko lililoko Ngong kaunti ya Kajiado kufuatia makabiliano kuhusu ardhi ya jamii inayozozaniwa ya Keekonyokie. Wakati wa tandabelua hilo, gari liliteketezwa na watu kadhaa wakajeruhiwa, huku barabara zikifungwa kufuatia makabiliano baina ya pande mbili. Ardhi hiyo yenye ukubwa wa ekari 2,682 na inayokadiriwa kuwa ya thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 100, imekumbwa na mzozo mkali kuhusiana na shughuli ya utoaji hatimiliki, huku pande mbili zikitofautiana licha ya uamuzi wa mahakama kuhusiana na suala hilo.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive