- 2,525 viewsDuration: 1:51Viongozi wa Upinzani wanasema watahakikisha wamesalia pamoja licha ya tofauti zao, hii ikiwa njia moja ya kung'oa mamlakani serikali ya Kenya Kwanza. Wakizungumza huko Makueni katika mazishi ya Mzee Philip Muteti Ndolo, viongozi hao wa upinzani wakiongozwa na kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka wamesema huu ni wakati wa kuweka taifa mbele ili kuwakomboa wakenya kutoka ufisadi na uongozi mbaya na pia kuokoa taasisi mbalimbali za kitaifa.