BBC News Swahili

  • | BBC Swahili
    786 views
    Leo katika Waridi wa BBC ,kimemulika maisha na mchango wa Bi. Khadija Mwanamboka, mwanamitindo mashuhuri kutoka Tanzania, ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko chanya ndani ya tasnia ya mitindo. Kwa zaidi ya miaka 25, Khadija amejitokeza kama mfano wa kuigwa, si tu kwa ubunifu wake bali pia kwa kazi yake ya kuwajengea uwezo wanawake nchini Tanzania. Ametumia majukwaa ya mitindo kama chombo cha kuwainua wanawake kiuchumi na kijamii, kupitia miradi na mafunzo mbalimbali. Katika juhudi za Tanzania kupata utambulisho wake wa kitaifa kupitia vazi rasmi, Bi. Khadija ameteuliwa kuwa mjumbe wa kamati maalum ya kuandaa vazi la taifa. Katika mahojiano na mwandishi wa BBC @elizabethkazibure amefichua baadhi ya siri na vigezo vilivyozingatiwa katika kubuni vazi hilo, vikiwemo rangi za bendera ya Tanzania, na usasa wa Mtanzania. - - 📹@frankmavura @enamuhisa #bbcswahili #mitindo #fashion #khadijamwanamboka #vazilataifa #watoto #wanawake Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw