USALAMA ZIWANI NAKURU
Shirika la huduma kwa wanyama pori la KWS pamoja na tume ya kutetea haki za bindamu nchini zilikabiliana vikali mbele ya kamati moja ya seneti kuhusiana na madai kwamba maafisa wa shirika hilo wanatumia nguvu kupita kiasi katika ziwa Nakuru. Tume hiyo ya haki za binadamu iliwasilisha ripoti kwa kamati ya usalama na ulinzi ya bunge la seneti iliyodai kwamba maafisa wa KWS wanawadhulumu na kuwatia nguvuni kiholela raia, kwa madai ya kuvua samaki bila idhini katika ziwa Nakuru,madai ambayo yalikanushwa vikali na mkurugenzi wa shirika la KWS Erastus Kanga. Kulingana na ripota wetu bungeni Gichuki Wachira, kamati hiyo ya seneti sasa inataka samaki kwenye ziwa Nakuru kufanyiwa upya utafiti kubaini iwapo ni salama kwa matumizi ya binadamu.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive