- 5,505 viewsDuration: 3:16Wizi wa simu hapa Nairobi na maeneo mengine nchini umeendelea kuwa donda sugu huku simu hizo sasa idara ya DCI ikibaini kuishia nchi za Tanzania, Uganda , Rwanda na hata Burundi. Katika operesheni ya kuwanasa wahusika ,eneo la Kericho lilipatikana kuwa eneo wanalotumia sana kusafisha mfumo wa simu hizi baada ya kuibwa . Mshukiwa mmoja amekamatwa na simu zaidi ya ishirini kunaswa pamoja na vifaa vya kusafisha mfumo wa simu hizo.