- 2,046 viewsDuration: 2:45Kundi la waangalizi wa uchaguzi la Elections Observation Group limesema lina wasiwasi kuhusu uadilifu wa uchaguzi mdogo wa hapo kesho katika eneo bunge la Ol Kalou. ELOG inadai ina ushahidi unaoonyesha ukiukaji mkubwa wa sheria za uchaguzi wakati wa maandalizi na kampeni, na sasa inaitaka Independent Electoral and Boundaries Commission kufanya uamuzi wa haraka kuhusu iwapo uchaguzi huo unapaswa kuendelea au kusitishwa, siku moja kabla ya wapiga kura kurejea debe kumchagua mbunge wao mpya.