Skip to main content
Skip to main content

Familia moja Bibirioni, Kiambu yaomba msaada wa shilingi 4.5M za matibabu ya figo ya mpendwa wao

  • | KBC Video
    130 views
    Duration: 3:45
    Familia moja katika eneo la Bibirioni, kaunti ya Kiambu inatoa wito wa msaada wa kifedha wa shilingi Milioni-4.5 zitakazofanikisha upandikizaji wa figo wa mpendwa wao. Jonathan Kimani Waroja, mwenye umri wa miaka-21, aligunduliwa kuwa na matatizo ya figo mwaka-2024, hali ambayo baadaye ilidorora na kusababisha figo yake kukosa kufanya kazi mwezi Disemba mwaka uliopita. Ni hali ambayo imempa mahangaiko tele kwani anategemea matibabu ya usafishaji damu mara mbili kila wiki ili aweze kuishi. Madaktari wamemshauri kufanyiwa matibabu hayo ya dharura kama suluhu ya kudumu kwa hali yake. Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV Check our website: https://www.kbc.co.ke/ #kbcchannel1 #news #kbclive