- 3,035 viewsDuration: 2:53Familia moja eneo la Kiembeni kaunti ya Mombasa inalilia haki baada ya mpendwa wao kufariki katika hali ya kutatanisha. Rachel Opiyo alimuaga mamake na kwenda kufanya ajira ya nyumbani kwa afisa mmoja wa polisi huko Mombasa, lakini alifanya kazi hiyo kwa siku moja tu kabla ya kufariki. Sasa familia yake inataka washukiwa, akiwemo afisa wa polisi katika kituo cha polisi cha Bandari na mkewe, wakamatwe ili kusaidia kufichua ukweli kuhusu kiini cha kifo cha binti yao.