- 3,567 viewsDuration: 2:32Familia moja kijiji cha Enchoro kaunti ya Nyamira inadai haki kwa jamaa yao aliyefariki baada ya kudai kuvamiwa na naibu chifu wa eneo hilo. Eric Mokaya anadaiwa kufumaniwa mwezi Disemba, na kupata majeraha yaliyosababisha kifo chake. Hata hivyo, naibu chifu amepinga madai ya kumvamia mwanaume huyo licha ya ripoti ya uchunguzi wa mwili kuonyesha kuwa kifo cha Mokaya kilitokana na kupigwa na kifaa butu kichwani