- 238 viewsFamilia Ya Virginia Njeri inayoishi eneo la Ruai kaunti ya Nairobi inakumbana na changamoto mara mbili. Kwanza nyumba yao imejaa maji kufuatia mvua kubwa inayoendelea kunyesha, na pili kifo cha mumewe Njeri kufuatia ajali ya barabarani. Sasa familia ya mama huyu imesalia kupanga mazishi katika nyumba iliyojaa maji.