Maelfu ya wakenya leo walifurika katika hifadhi ya kitaifa ya wanyama pori jijini Nairobi kusherehekea sikukuu ya Krismasi kwa mtindo wa kipekee. Kwa wengi wao, ilikuwa ni mazingira tulivu na ya kuburudisha mbali na shamrashamra na pilikapilika za kawaida za jiji. Usimamizi wa hifadhi hiyo, ambao umeandaa huduma za mabasi kwa wageni ndani ya hifadhi, wamesema wanatarajia kuendelea kushuhudia idadi kubwa ya Wakenya wakitembelea hifadhi hiyo hadi tarehe mbili mwezi Januari mwakani.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive