- 648 viewsDuration: 3:06Tume ya kitaifa ya haki za binadamu nchini Kenya inasema huenda mpango wa kuwalipa fidia wahanga wa dhulma, ikiwemo waathiriwa wa maandamano ya Gen Z ya mwaka 2024, ukachelewa kutekelezwa kutokana na wizara ya fedha kuchelewesha fedha za ukusanyaji na uhakiki wa taarifa. Tume hiyo inasema imepokea majina ya watu 1,525 pekee kufikia mwisho wa zoezi hilo, huku wengi wa waathiriwa wakiwa bado hawajatambuliwa kutokana na ukosefu wa fedha.