- 1,396 viewsDuration: 2:55Wakenya waliofika kutafuta huduma katika hospitali za kibinafsi wakitumia bima ya SHA wamesalia njiapanda kufuatia hatua ya hospitali hizi kusitisha huduma zake kupitia bima hii ya serikali. Muungano wa hospitali za mashinani, mjini na zile za kibinafsi RUPHA ilisema imechukua hatua hii kwa kuwa serikali haijalipa deni. Baadhi ya wagonjwa wamelazimika kurudi nyumbani bila matibabu kwa kukosa pesa