Rais William Ruto leo amejumuika na familia ya marehemu mbunge wa Olkalou David Kiaraho kwa ibada ya mazishi. Katika hafla hiyo, familia ilimtaja Kiaraho kama kiongozi aliyependa na kuilinda familia yake na aliyejali maslahi ya wananchi wa eneo la Olkalou. Mbali na Rais Ruto ibada ya mazishi pia imehudhuriwa na naibu rais Kithure Kindiki, aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua miongoni mwa viongozi wengine. Kiaraho alifariki wakati akipokea matibabu Nairobi Hospital mwezi machi baada ya kuugua kwa muda mrefu.