- 770 viewsDuration: 3:23Wakristo nchini Kenya leo waliungana na ulimwengu kuadhimisha Jumapili ya Pasaka huku viongozi wa kidini wakiwataka wanasiasa kukomesha kampeni za mapema na siasa za kukoseana heshima. Askofu Mkuu wa kanisa la katoliki dayosisi ya Nairobi Phillip Anyolo akisema kuwa siasa za mapema zinalemaza maendeleo huku mwenzake wa kanisa la Kianglikana Jackson Ole Sapit katika ujumbe wake, akiwahimiza wakristo kuwa na matumaini ya mwanzo mpya wa nchi.