- 3,819 viewsDuration: 3:07Inspekta Jenerali wa Polisi Douglas Kanja na Mkurugenzi wa DCI Mohamed Amin wameagizwa kwa mara ya pili kufika mahakamani kueleza waliko vijana watatu waliotoweka kabla na wakati wa maadhimisho ya Juni 25. Maafisa hao walitarajiwa kufika mahakamani leo lakini hawakufika, huku wakili wao akieleza kuwa walikuwa kwenye mkutano muhimu wa kupanga masuala ya kiusalama. Wakati huo huo, familia za vijana hao zimeendelea kulilia haki na kutaka wapendwa wao warejeshwe nyumbani baada ya kutoweka kwa zaidi ya wiki tatu.