- 324 viewsDuration: 4:15Kasisi wa Dayosisi ya A.C.K Kitale amevutia hisia za wengi hasa wapenzi wa burudani kutokana na mtindo wake usio wa kawaida wa kutoa huduma, akipeleka injili nje ya madhabahu hadi kwenye vilabu vya usiku. Padre Michael Watenga amekuwa akitumia mbinu ya kipekee ya kuwatafuta anaowaita kondoo waliopotea akifanya ziara katika maeneo ya burudani kote nchini. Ingawa mbinu zake zimekosolewa na baadhi, kasisi huyo ameendelea kusimama imara na kutetea njia yake.