- 1,748 viewsDuration: 2:00Viongozi wa Kenya Kwanza wameeleza wasiwasi wao kuhusu idadi ndogo ya wapiga kura waliojitokeza kujiandikisha katika baadhi ya maeneo ya Bonde la Ufa. Wakizungumza wakati wa ziara katika Kaunti ya Nandi, wanasiasa hao wameonya kuwa idadi ndogo ya wakazi wanaojisajili kupiga kura katika eneo hilo linalochukuliwa kuwa ngome ya kisiasa ya Rais William Ruto inaweza kudhoofisha nafasi yake ya kupata ushindi mkubwa katika uchaguzi mkuu ujao.