Kenya inaongoza juhudi za kuweka masharti ya mikopo kwenye mfumo wa dijitali na kuyawianisha ili yaendane na yale ya mataifa wanachama wa shirika la COMESA katika juhudi za kurahisisha upatikanaji wa mikopo kwa wajasiriamali. Akizungumza na runinga ya Channel 1, katibu katika idara ya ustawi wa biashara ndogo na zile za kadri Susan Mang’eni, alisema kuwa kuwianisha viwango hivyo kutawawezesha wafanyabiashara kupata mikopo kutoka nchi nyingine na pia kupunguza urasimu katika sekta ya fedha katika kanda hii.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive