- 1,938 viewsDuration: 2:58Maandalizi ya uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Ol Kalou yamekamilika huku zaidi ya wapiga kura elfu 70 wakitarajiwa kushiriki uchaguzi huo hapo kesho. Saa chache kabla ya uchaguzi huo, mamia ya maafisa wa usalama wameimarisha doria katika eneo bunge hilo, siku moja baada ya serikali kutangaza kuwatuma zaidi ya maafisa 1,000 kusimamia usalama na kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani.