- 3,736 viewsDuration: 2:57Mvua kubwa inayoendelea kunyesha huko Mombasa imesababisha mafuriko katika barabara nyingi za Nyanjani na maji kuingia katika makazi. Katika mitaa ya Ziwa la Ng’ombe, Bamburi na Kadzandani, biashara zimeathirika, zahanati kusalia kufungwa pamoja na kituo cha polisi cha Kadzandani. Aidha, wakazi wameshindwa kufika katika baadhi ya maeneo kutokana na mafuriko barabarani. Wakazi sasa wanataka mabomba ya maji taka kurekebishwa kwa haraka.