- 368 viewsDuration: 1:35Magavana wameibua hisia kali wakipinga mfumo mpya wa ununuzi na kutoa kandarasi kidijitali wakisema umefeli miezi mitatu baada ya kuanza kutekelezwa. Kadhalika, wanataka mgao wa fedha wa shilingi bilioni 36 ambazo hawajapokea hadi sasa. Magavana hao wameibua hoja hizo katika mkutano wa 28 wa bajeti baina ya serikali kuu na serikali za kaunti unaoongozwa na naibu wa rais katika makao yake rasmi ya Karen.