- 434 viewsDuration: 1:30Serikali imeanza kutoa hatimiliki kwa wakazi zaidi ya 1,000 waliokuwa wakiishi kama maskwota katika eneo la Chelimo, Kaunti ya Kericho. Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, Katibu wa wizara ya Ardhi Nixon Korir alisema kuwa mpango huo utafungua fursa za kiuchumi na kuboresha maisha ya wakazi wa eneo hilo. Kwa upande wake, Gavana wa Kericho Erick Mutai alieleza matumaini yake kuwa hatua hiyo itachochea ukuaji wa mji huo na kuvutia wawekezaji.