Matumizi ya bangi yaongezeka kwa asilimia 90 katika kipindi cha miaka tano

  • | K24 Video
    57 views

    Utafiti mpya wa mamlaka ya kudhibiti matumizi ya pombe na dawa za kulevya (NACADA) umedhibitisha kuwa matumizi ya bangi yameongezeka kwa asilimia 90 katika kipindi cha miaka 5 iliyopita humu nchini. Ni utafiti uliojumuisha watu 3,314 wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35, wengi wa wanaotumia bangi wakiwa vijana ambao wanadhania kuwa matumizi yake hayana athari za kiafya ikilinganishwa na dawa nyingine za kulevya au pombe