- 30,962 viewsDuration: 56sMeli mbili za kubeba mafuta zimeteketea kwa moto baada ya kushambuliwa huko karibu na pwani huko Iraq. Mamlaka za Iraq zimesema mfanyakazi mmoja wa meli aliuawa na wengine 38 waliokolewa baada ya meli hizo kushambuliwa na boti za Iran zilizokuwa zimejazwa vilipuzi. Tukio hilo limetokea saa chache tu baada ya meli nyingine tatu kushambuliwa katika Ghuba ya Uajemi. Kundi la Islamic Revolutionary Guard la Iran lilidai kuhusika na moja ya mashambulizi hayo. #bbcswahili #foryou #fyp Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw