- 798 viewsDuration: 2:55Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Renson Igonga ameshutumu Mamlaka ya kuangazia utendakazi wa polisi IPOA na idara ya upelelezi DCI kwa kukosa kuwasilisha ushahidi muhimu kuhusu kesi za madai ya polisi kukiuka sheria. Akizungumza jijini Nairobi alipozindua mtaala kuhusu mashtaka ya ugaidi Igonga amesema kesi nyingi ambazo hazijakamilishwa zinawahusu maafisa wa usalama. Miongoni mwa kesi hizo ni kisa cha polisi kudaiwa kuwapiga risasi watu wawili mtaani Kitengela.