- 930 viewsMshukiwa aliyekamatwa kufuatia kifo cha Daktari Job Obwaka amefikishwa katika mahakama kuu ya Kibra. Mshukiwa huyo Beatrice Wangari tayari amefikishwa mahakamani huku Upande wa mashtaka ukitarajiwa kuomba muda zaidi kumzuilia. Marehemu Obwaka aliaga dunia siku ya ijumaa huko Kitengela.