Skip to main content
Skip to main content

Msichana akumbatia mti kwa zaidi ya saa 45 mjini Nyeri

  • | Citizen TV
    23,268 views
    Duration: 4:43
    Kama njia ya kuwarai wakenya kukumbatia uutunzaji wa mazingira, Truphena Muthoni binti mwenye umri wa miaka 22 yuko mbioni kujaribu kuvunja rekodi ya dunia ya kuukumbatia mti, zoezi alilolianza jumatatu adhuhuri. Binti huyo ambaye pia ni mwanamazingira, ameukumbatia mti mmoja kwenye ofisi za gavana wa kaunti ya nyeri kwa saa 45 sasa, lengo likiwa ni kuukumbatia mti huo kwa zaidi ya saa 72.