Mtaalamu wa fedha mwenye miaka 13 kutoka Tanzania

  • | BBC Swahili
    865 views
    Je ulianza kutunza akiba ya pesa ukiwa na umri wa miaka mingapi? Tracy Rabi ni mtaalam wa masuala ya fedha mwenye umri wa miaka 13 kutoka Tanzania. Alianza kujifunza masuala ya fedha akiwa na umri wa miaka nane na sasa ana malengo ya kusaidia watoto wengine kuwafundisha kuhusu fedha na ujasiriamali. Tracy Rabi ameandika vitabu vitatu vinavyohusu pesa na ujasiriamali na anaendesha mafunzo ya biashara kwa watoto yote haya akiwa na umri wa miaka 13 tu. #bbcswahili #tanzania #watoto Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw