- 9,303 viewsDuration: 2:59Polisi kaunti ya Machakos wameanzisha uchunguzi wa kifo cha ghafla cha mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya upili ya Katoloni. Mwanafunzi huyo Consolata Ndiku anaripotiwa kuugua akiwa shule na kukimbizwa hospitalini alikoripotiwa kufariki alipofikishwa. Familia sasa ikisema ina maswali kuhusu chanzo cha kifo cha binti waliyemtaja kuwa kwenye hali njema ya kiafya.