Naibu Rais prof kithure Kindiki, ameirai idara ya mahakama kuondoa amri ya kuzuia kutekelezwa kwa Sheria mpya za barabarani zinazohusisha faini za papo hapo, kama njia ya kuzuia ajali zinazoendelea kushuhudiwa nchini
Akitoa wito huo alipohudhuria ibada ya wafu ya watu 16 waliofariki Kwenye ajali iliyotokea kwenye barabara ya Nyeri kuelekea Mweiga, Kindiki amewarai madereva kuwa waangalifu zaidi barabara na kuzingatia mwendo wanaoendesha magari.
Wakati huo huo, Serikali imetakiwa kujenga njia mbadala ya matumizi Kwa waendesha baiskeli Kwenye barabara hio, ajali hii ikitajwa kutokea dereva alipokuwa anakwepa kumgonga mwendesha baiskeli..