- 840 viewsDuration: 3:31Serikali ilitangaza oparesheni mpya ya kiusalama ya kukabiliana na wezi wa mifugo na majangili katika kaunti za Isiolo, Samburu na Meru. Waziri wa usalama Kipchumba Murkomen, alisema oparesheni hiyo ya pamoja itahusisha wanajeshi wa KDF na shirika la kitaifa la ujasusi (NIS). Murkomen alisema vyombo hivyo vitafanya kazi kwa ushirikiano na polisi kuwaondoa majangili na kumaliza kabisa uhalifu katika maeneo hayo.