- 1,978 viewsDuration: 3:18Mtu mmoja alijeruhiwa kwa kudungwa kisu baada ya makundi mawili ya wahuni kukabiliana kwenye mazishi katika eneo la Ikolomani, kaunti ya Kakamega. Purukushani ziliibuka baada ya mwakilishi wa kike wa kaunti hiyo Elise Muhanda kuzimiwa kipaza sauti. Inaarifiwa kuwa makundi ya wafuasi wa gavana wa Kakamega Fernandes Barasa na mwakilishi wa kike yalikabiliana na kulazimisha mwili wa marehemu kuondolewa ghafla.