Rais William Ruto amehitimisha ziara yake ya kikazi ya siku nne katika eneo la South Rift, ambapo alichukua fursa hiyo kuukosoa upande wa upinzani , kwa kile alichokitaja kuwa kuendeleza siasa za mgawanyiko na kukosa ajenda. Rais Ruto ambaye alizindua miradi kadhaa pamoja na kukagua miradi inayoendelea, aliuhimiza upande wa upinzani uelezee ajenda yao ya maendeleo badala ya kukosoa serikali kila mara. Amesisitiza kuwa serikali yake haitayumba katika kuandaa mpango wa maendeleo wa nchi. Mwanahabari wetu Timothy Kipnusu ana taarifa kuhusu ratiba ya rais katika siku ya mwisho ya ziara yake.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive