- 3,715 viewsDuration: 3:08Rais William Ruto leo kwa siku ya nne ameendelea kukutana na makundi mbalimbali katika ikulu ya Nairobi, leo hii akikutana na maafisa wa usalama wa kibinafsi. Kwenye kikao hicho. Rais ameagiza jina la 'Watchman' au bawabu kuondolewa kutoka kwenye sera na stakabadhi zote za serikali akisema kwa sasa wahudumu hao watambuliwe kama maafisa wa usalama wa kibinafsi. Rais ameendelea kutoa ahadi chungu nzima kwa wageni wake huku akipigia debe safari yake ya ikulu ya mwaka ujao