Rais William Ruto amewakosoa viongozi wa upinzani, na haswa kinara wa DCP Rigathi Gachagua , kuhusu ziara yake katika eneo la kaskazini na haswa mikakati ya serikali ya kukabili ukame katika eneo hilo. Rais Ruto amesema kuwa viongozi hao hawana ufahamu kuhusu mahitaji ya wakazi wa maeneo hayo akisisitiza miradi mbalimbali ya serikali ya kukabili janga la ukame kaskazini mwa nchi. aidha rais Ruto amesema kuwa nia yake ni kuhakikisha kuwa wakazi wa maeneo hayo wanapata maendeleo sawa na wenzao kwingineko.