- 15,625 viewsDuration: 2:52Mamlaka ya kuchunguza utendakazi wa maafisa wa polisi IPOA na kitengo cha kuwachunguza maafisa wa polisi IAU, zimeanzisha uchunguzi wa kubaini iwapo maafisa wa polisi walihusika kwenye shambulizi la kanisa la ACK Witima wakati wa ibada iliyokuwa ikihudhuriwa na kinara wa DCP Rigathi Gachagua siku ya Jumapili. Mratibu wa eneo la kati Joshua Nkanatha, amewarai maafisa wa polisi na wale wa utawala kutojihusisha na ghasia na kuwataka kuzingatia kanuni zinazoongoza utendakazi wao. Kamau Mwangi anaarifu.