- 4,620 viewsDuration: 1:48Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna anasisitiza kuwa yeye bado ndiye katibu mkuu wa chama cha ODM. Akizungumza siku moja baada ya baraza kuu la odm kuafikia kumtimua, sifuna anasema kuwa uamuzi huo haukuwa wa kisheria, na kuapa kupigana jino na ukucha mahakamani kupinga uamuzi huo. Aidha viongozi mbalimbali wa odm wanaunga mkono kauli ya sifuna wakitaja yaliyotendeka kama ukandamizaji mkubwa na mapinduzi.