Uandaaji wa sherehe za kitaifa nje ya jiji la Nairobi ulioanza mwaka 2016, umewezesha kaunti kupata sio tu manufaa ya kiuchumi, bali pia miradi ya maendeleo ya kudumu. Katika kaunti ya Kitui iliyoandaa sherehe ya siku kuu ya Mashujaa leo, uwanja wa michezo wa Ithookwe wenye uwezo wa kusitiri watu elfu 10, ulijengwa kwa ajili ya sherehe hiyo ya kitaifa, na pia Ikulu ndogo kujengwa katika eneo hilo. Gavana wa Kitui Julius Malombe alitaja sherehe hiyo kuwa hatua kubwa katika kuifungua kaunti hiyo kwa maeneo mengine ya nchi.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive