- 4,021 viewsDuration: 3:14Viongozi wa upinzani wamewarai wakaazi wa Mombasa kupinga utawala mbaya wa kaunti hiyo na kusema kwa miaka mingi, hatma ya uongozi wa eneo hilo imeamuliwa na watu kutoka familia moja. Viongozi hao wamemuunga mkono mbunge wa Nyali, Mohammed Ali, kugombea kiti cha ugavana wa Mombasa kwa tiketi ya chama cha Wiper, wakisema kuwa wakati umewadia kwa wakazi wa Mombasa kufanya mabadiliko yatakayowaletea manufaa.