- 5,042 viewsDuration: 3:22Video zinazomuonyesha Mbunge wa Nyaribari Chache Zaheer Jhanda akigawa fedha kwa wakazi zimeibua hisia tofauti miongoni mwa Wakenya, wengi wakisema hatua hiyo inadhalilisha hadhi ya wananchi na kudhoofisha uhuru wa wapiga kura. Mashirika ya kijamii sasa yanaitaka Tume ya Uchaguzi IEBC kuingilia kati, kudhibiti matukio hayo na kusitisha kampeni za mapema.