- 7,757 viewsDuration: 3:20Viongozi wa mrengo wa Linda Mwananchi wamempa Katibu wa usalama wa kitaifa Raymond Omollo wiki mbili kujizulu wakisema alihusika na kushambuliwa na kujeruhiwa kwa Seneta wa Vihiga Godfrey Osotsi siku nne zilizopita huko Kisumu. Viongozi hao walikuwa wakizungumza baada ya Seneta Osotsi kuondoka hospitalini alikokuwa akipokea matibabu. Seneta Osotsi amesema kabla ya tukio hilo alikuwa akifuatwa na baadhi ya wahusika waliopanga njama ya kumshambulia.