- 5,048 viewsDuration: 3:29Viongozi kutoka maeneo ya kaskazini mashariki wamekashifu vikali machafuko yanayoendelea eneo la Mwingi, na kutaka asasi za usalama kuwajibika na kuimarisha doria. Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka ameongoza viongozi wengine kuwarai wakazi kusitisha mapigano akisema kuwa ulipishaji kisasi hautasaidia. Haya ni huku Baraza la viongozi wa dini ya kiislamu -SUPKEM- inawanyoshea kidole cha lawama baadhi ya viongozi kwa kuchochea vita hivyo na kupinga madai kuwa ni vita kati ya wafugaji na wakulima