- 198 viewsDuration: 3:04Washikadau katika taaluma ya uanahabari barani Afrika wamepinga wito wa serikali kusaidia kifedha vyombo vya habari vya kiasili, wakisema badala yake serikali ilinde uhuru wao na kuwawezesha kujitegemea katika enzi ya mabadiliko ya kidijitali. Katika kongamano la Pan African Media linalofanyika jijini Nairobi, wadau wameeleza kuwa jukumu kuu la vyombo vya habari sasa ni uhakiki wa taarifa ili kupambanua taarifa za kweli na zile bandia.