- 168 viewsShughuli ya kutoa maoni kuhusu mswada wa fedha wa mwaka wa 2026 iliendelezwa katika kaunti za Nairobi, Siaya na Makueni huku wakazi wakielezea wazi hisia zao kuhusu ushuru wa bidhaa na huduma muhimu. Wakazi waliofika mbele ya kamati ya bunge kuhusu fedha na mpango waliitaka serikali kuwahakikishia kwamba itakomesha ufisadi na utumizi mbaya wa rasilmali, kabla ya mapendekezo yoyote ya ushuru mpya.