Maafisa wa polisi wa kituo Cha Baricho eneo la Ndia, Kaunti ya Kirinyaga,wamelazimika kuwakabili waandamanaji waliofunga barabara ya Kiburu-Kabonge. Waandamanaji hao walifunga barabara hiyo Kwa kuwasha moto barabarani kulalamikia kuchelewa kwa ujenzi wa daraja la Njoga-Kariani kwenye mto Rwamuthambi.Wakaazi hawa, wanalalamikia kugharamika zaidi kusafirisha mazao yao sokoni, wakiwalaumu viongozi kwa kuwapuuza. Mbunge wa eneo hilo George Kariuki amewahakikishia wakazi kuwa shilingi milioni 24 zimetengwa kwa ujenzi wa daraja hilo.