- 204 viewsWakulima katika kaunti ya uasin gishu wanahofia kuwa mazao yao yataharibikia shambani kutokana na uhaba wa mbole. Hii leo, Mamia ya wakulima waliandamana mjini Eldoret wakilalamika kuwa ukosefu wa mbolea ya kunyunyizia mahindi unawasababisha kugharamikia safari za kila mara kwenye maghala ya NCPB bila mafanikio. Aidha wanahofia kuwa hali hiyo itaathiri utoshelevu wa chakula kwenye eneo hilo ambalo ni mojawapo ya maghala ya taifa.